Habari

MIFUMO YA KIELEKTRONIKI KUBORESHA HUDUMA ZA SEKTA YA ARDHI- NDEJEMBI

  • 31 Oct, 2024
MIFUMO YA KIELEKTRONIKI KUBORESHA HUDUMA ZA SEKTA YA ARDHI- NDEJEMBI

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Deogratius Ndejembi amesema Wizara yake imeanzisha mifumo ya kielektroniki ya kusimamia sekta ya Ardhi ikiwemo e-Ardhi ili kutoa huduma bora kwa Watanzania.

 

Waziri Ndejembi amesema hayo wakati akifungua mafunzo ya Mifumo inayosimamia Sekta ya Ardhi kwa Kamati ya Mawasiliano, Ardhi na Nishati ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Oktoba 30, 2024 Dar es Salaam.

 

Wajumbe wa Kamati hiyo na Watendaji wa Wizara ya Ardhi Zanzibar wamefanya ziara maalum kwa ajili ya kujifunza na kubadilishana uzoefu wa namna ya mifumo ya TEHAMA ya Ardhi ya Tanzania Bara inavyofanya kazi katika kuwahudumia Wananchi.