Kurasa

MAJUKUMU

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inayo majukumu yafuatayo:

  • Kuratibu na kusimamia utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Ardhi na Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Makazi;
  • Kusimamia Utawala wa Ardhi;
  • Kusimamia upangaji na uendelezaji wa miji na vijiji;
  • Kusimamia na kuwezesha upimaji wa ardhi na kutayarisha ramani;
  • Kumilikisha ardhi na kuwezesha utoaji wa hati za hakimiliki ya kimila;
  • Kusajili hatimiliki za ardhi, miamala na nyaraka za kisheria;
  • Kusimamia uthamini wa mali;
  • Kuhamasisha na kuwezesha ujenzi wa nyumba bora;
  • Kusimamia uendelezaji milki;
  • Kusimamia utatuzi wa migogoro ya ardhi;
  • Kusimamia utunzaji wa kumbukumbu za ardhi;
  • Kusimamia ukusanyaji wa maduhuli yatokanayo na huduma za Sekta ya Ardhi; na
  • Kuwezesha uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi na kufuatilia utekelezaji wake