Kurasa
Idara ya TEHAMA
Majukumu ya idara ni pamoja na: -
i. Kubuni, kuendeleza na kudumisha miundombinu na mifumo ya Tehama;
ii. Kutoa ushauri wa kitaalamu na msaada wa kiufundi kuhusu Tehama na usimamizi wa taarifa na takwimu;
iii. Kuchambua huduma za kielektroniki na kuwezesha matumizi ya Serikali Mtandao (e-Government) ndani ya Wizara;
iv. Kuratibu masuala ya usimamizi wa taarifa na takwimu katika ofisi zote za Wizara;
v. Kuandaa Mkakati wa Tehama wa Taasisi kwa ujumla na Mpango wa Utekelezaji wake;
vi. Kuandaa Miundombinu ya Kisanifu ya Tehama ikijumuisha Usanifu wa Taasisi (Enterprise Architecture), Programu-tumizi, Mitandao/Teknolojia na Usalama wa TEHAMA;
vii. Kutoa huduma za msaada wa TEHAMA kwa watumiaji wote, kuandaa miongozo ya matumizi ya TEHAMA na kufuatilia utekelezaji wake;
viii. Kubuni na kuratibu mafunzo ya Tehama na kujenga uwezo wa watumishi wa TEHAMA katika ngazi zote; na
ix. Kutambua, kuchambua na kutatua changamoto (troubleshooting) za mifumo ya TEHAMA (programu-tumizi na miundombinu) na kutoa suluhisho stahiki.