Kurasa
Kitengo cha Ununuzi Serikalini
Majukumu ya Kitengo ni kama ifuatavyo: -
i. Kuandaa Mpango wa Ununuzi wa Mwaka wa Wizara;
ii. Kuishauri Menejimenti ya Wizara kuhusu masuala yanayohusu ununuzi wa bidhaa na huduma, pamoja na usimamizi wa vifaa na usafirishaji;
iii. Kufuatilia uzingatiaji wa taratibu na michakato ya ununuzi kwa mujibu wa Sheria ya Ununuzi wa Umma;
iv. Kununua, kutunza na kusimamia vifaa, mali na huduma ili kukidhi mahitaji ya uendeshaji na ugavi wa Wizara;
v. Kuandaa, kuhifadhi na kusasisha orodha ya mali na vifaa vya Wizara;
vi. Kutoa huduma za sekretarieti kwa Bodi ya Zabuni kwa mujibu wa Sheria ya Ununuzi wa Umma; na
vii. Kuweka viwango vya bidhaa na huduma zitakazonunuliwa na kufuatilia uzingatiaji wake ili kuhakikisha thamani halisi ya fedha (value for money).