Kurasa

Kitengo cha Huduma za Kisheria

Majukumu ya Kitengo cha Sheria ni pamoja na: -

i. Kutoa ushauri wa kisheria na msaada wa kitaalamu kwa Idara, Vitengo na taasisi zilizo chini ya Wizara;

ii. Kusimamia na kuendesha mashauri ya madai ya kiraia na mashauri mengine yanayofunguliwa na au dhidi ya Wizara, kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali;

iii. Kuandaa na kupitia (kuhakiki) mikataba;

iv. Kuandaa na kuhifadhi rejista ya sheria na kanuni zote zinazosimamiwa na kutekelezwa na Wizara;

v. Kusimamia mapitio ya sheria husika na kupendekeza marekebisho yanayohitajika au uundwaji wa sheria mpya;

vi. Kuandaa Kanuni, Sheria Ndogo (Rules) na Tangazo la Serikali;

vii. Kuarifu na kuifahamisha Wizara kuhusu sheria mpya zilizotungwa au marekebisho ya sheria yanayohusiana na majukumu ya Wizara; na

viii. Kuandaa na kuhifadhi rejista ya mashauri yote yanayofunguliwa na au dhidi ya Wizara katika Mahakama ya Rufaa, Mahakama Kuu na Mabaraza (Tribunals).