Kurasa

Kitengo cha Uhasibu na Fedha

Majukumu ya Kitengo ni pamoja na: -

i. Kuhakikisha kuwa Fedha za umma zinazotengwa kwa ajili ya matumizi ya Kawaida, Maendeleo na Amana zinatumika kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia Fedha za Umma;

ii. Kuhakikisha kuwa malipo ya watumishi wa Wizara na Wadau yanalipwa kwa wakati;

iii. Kuhakikisha kuwa Fedha za maduhuli ya Serikali (mapato) zinakusanywa ili kufikia malengo;

iv. Kuandaa Hesabu na Taarifa za Fedha za Wizara; na

v. Kusimamia na kuratibu hoja za ukaguzi.