Kurasa

Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini

Majukumu ya Kitengo ni kama ifuatavyo: -

i. Kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa Mipango ya Mwaka na Mpango Mkakati wa Wizara;

ii. Kuandaa taarifa za mara kwa mara za utekelezaji na utendaji;

iii. Kutoa mchango katika maandalizi ya mipango, programu na shughuli za bajeti pamoja na uanzishaji wa viashiria vya utendaji;

iv. Kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu mchakato wa Ufuatiliaji na Tathmini (M&E);

v. Kufanya tafiti kuhusu athari za mipango, miradi na programu zinazotekelezwa na Wizara;

vi. Kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) katika ukusanyaji wa takwimu, uingizaji/uchakataji wa data, uchambuzi na tafsiri;

vii. Kutoa msaada wa kitaalamu wa takwimu wakati wa maandalizi ya mipango na bajeti;

viii. Kuwa msimamizi na kitovu cha takwimu za Sekta;

ix. Kufanya tafiti za utoaji wa huduma ili kukusanya maoni ya wadau/wateja kuhusu huduma zinazotolewa;

x. Kuratibu mapitio ya utendaji ya nusu mwaka na ya mwaka mzima;

xi. Kuratibu utekelezaji wa mikataba ya utendaji (Performance Contracting); na

xii. Kufuatilia utendaji wa Wakala za Serikali, Mashirika ya Umma na Mashirika ya Kisheria yaliyo chini ya Wizara.