Kurasa

Kitengo cha Usajili wa Hati

Majukumu ya Kitengo ni pamoja na: -

i. Kusajili hati na miamala mingine (usajili wa baadaye) ya ardhi kwa mujibu wa Sheria ya Usajili wa Ardhi (Sura ya 334);

ii. Kusajili nyaraka za lazima na za hiari kwa mujibu wa Sheria ya Usajili wa Nyaraka (Sura ya 117);

iii. Kusajili chattels/vyombo (vya kuhamishika/kukodishwa kifedha) kama vile samani, magari, ndege, meli, n.k. kwa mujibu wa Sheria ya Uhamisho wa Chattels (Sura ya 210);

iv. Kutoa ripoti rasmi za utafutaji na kuhifadhi nyaraka kwa maombi;

v. Kuwa na dhamana ya kuhifadhi hati zote na miamala iliyosajiliwa;

vi. Kusimamia, kuanzisha na kuendesha ofisi za usajili wa ardhi;

vii. Kusimamia na kuratibu usajili wa nyaraka na miamala ya ardhi nchini kote kupitia Ofisi za Utawala wa Ardhi za Kanda;

viii. Kufuatilia na kutathmini utendaji wa ofisi za Msajili wa Hati katika Kanda;

ix. Kupitia sheria za usajili na kupendekeza hatua stahiki za marekebisho na mapitio;

x. Kuhudhuria mahakamani pale inapoitwa au kuombwa kwa amri ya mahakama kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu;

xi. Kusajili rehani (mortgages); na

xii. Kusajili hati za umiliki wa vitengo na miamala kwa mujibu wa Sheria ya Hati za Vitengo ya mwaka 2008.