Kurasa

Idara ya Sera na Mipango

Majukumu ya Idara ni pamoja na: -

i. Kuratibu uandaaji wa Sera za Wizara, kufuatilia utekelezaji wake na kuzifanyia tathmini na kuhakikisha zinaendana na mipango, sera na mikakati ya Kitaifa;

ii. Kuchambua nyaraka mbalimbali za Baraza la Mawaziri na kutoa maoni;

iii. Kuratibu uandaaji na utekelezaji wa Mipango na Bajeti ya Wizara;

iv. Kufanya ufuatiliaji na tathmini wa Mipango na Bajeti ya Wizara na kuandaa taarifa za utekelezaji wa Bajeti;

v. Kufanya utafiti, ufuatiliaji na tathmini ya mipango ya Wizara ili kuweka msingi wa kufanya maamuzi sahihi;

vi. Kuratibu maandalizi ya Hotuba ya Bajeti ya Wizara na mchango wa Wizara katika Taarifa ya Hali ya Uchumi;

vii. Kuratibu Utekelezaji wa Mikataba ya Utendaji Kazi;

viii. Kuhakikisha kuna kuwepo na ujuzi wa kutosha wa kutumia Mpango Mkakati, Mpango Kazi na Mpango wa Ufuatiliaji na Tathimini wa Wizara;

ix. Kuratibu utekelezaji wa ushiriki wa Sekta Binafsi Wizarani.