Habari

KAMATI YA BUNGE YAPOKEA TAARIFA YA WIZARA YA ARDHI

  • 12 Aug, 2026
KAMATI YA BUNGE YAPOKEA TAARIFA YA WIZARA YA ARDHI

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utali, ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Timotheo Mnzava, leo tarehe 11 Agosti 2026 bungeni jijini Dodoma imekutana na watendaji wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi wakiongozwa na Naibu Waziri, Mhe. Kaspar Mmuya, kwa ajili ya kupokea na kujadili taarifa kuhusu utendaji na usimamizi wa watumishi wa kada ya ardhi pamoja na hatua zilizofikiwa atika uanzishaji wa Kamisheni ya Ardhi.

 

Katika kikao hicho, Wizara imeieleza Kamati hatua mbalimbali zinazochukuliwa katika kuimarisha usimamizi wa watumishi wa sekta ya ardhi, kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma na kukabiliana na changamoto majukumu ya sekta hiyo.

 

Kikao hicho kimefanyika Bungeni Jijini Dodoma, ikiwa ni sehemu ya usimamizi wa Bunge katika kufuatilia utekelezaji wa majukumu ya Serikali katika sekta ya ardhi.

 

Naibu Katibu Mkuu Bi Lucy Kabyemera, wajumbe wa Menejimenti ya Wizara pamoja na wakuu wa Taasisi zikizochini ya wizara pia walishiriki katika kikao hicho.