Taarifa Muhimu

UFAFANUZI WA NOTISI ZILIZOTOLEWA KWA VIJIJI VYA OLOLOSOKWAN, SOITSAMBU, ENGUSEROSAMBU, ARASH NA LOSOITO

Wizara inapenda kutoa ufafanuzi kutokana na taarifa zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu notisi zilizotolewa tarehe 4 Juni,2026 na Ofisi ya Msajili wa Hati Mkoa wa Arusha kwa Vijiji vya Ololosokwan, Soitsambu, Enguserosambu, Arash na Losoito vilivyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro Mkoani Arusha.