1. Uthamini ni nini?
Uthamini ni utaratibu wa utaalam wa kukadiria na kushauri kuhusu thamani ya mali isiyohamishika (kama vile ardhi,majengo na mazao). Hivyo neno uthamini linatokana na neno thamani
2.Thamani ni nini?
Thamani kwa ujumla wake inaweza kuelezeka kama bei inayolipwa kwa ajili ya kupata kitu. Lakini kwa lugha ya kitaaluma: thamani hususan ya mali isiyohamishika kwa mfano ardhi, inahusisha;-
3.Je, Ardhi ina thamani?
Ndiyo, kwa sababu ardhi ni rasilimali ya msingi ambayo shughuli zote za kijamiii, kiuchumi na kimaendeleo zinafanyika juu yake. Kwa Tanzania, asilimia takriban themanini (80) ya wananchi wa vijijini hutegemea ardhi kwa maisha yao ya kila siku kwa chakula, kipato na mahitaji mengine.
· Ardhi humilikiwa kiserikali na kimila kwa sheria, kanuni na taratibu zinazokubalika. Ni kutokana na thamani ya ardhi watu hulazimika kumiliki ardhi na kuishi ndani yake.
4.Nini umuhimu wa uthamini?
Kuongezeka kwa ushindani wa mahitaji ya ardhi inayomilikiwa kiserikali, ikilinganishwa na ardhi iliyopo kumejenga umuhimu wa kusimamia na kutawala mali hiyo adimu kwa umakini mkubwa. Hivyo, uthamini ni nguzo mojawapo ya utawala na usimamizi bora wa ardhi kwa kuwezesha maamuzi ya maendeleo bora ya ardhi kufanyika.
5. Nini sababu ya uthamini?
Uthamini unaweza kutakiwa kwa madhumuni mbalimbali kama vile:
6.Uthamini kwa madhumuni ya fidia:
Dhana ya fidia:
Kwa kuwa ardhi ya Tanzania ni mali ya wananchi wote, Rais ndiye mwenye dhamana ya kulinda kwa manufaa ya wote. Hata hivyo mwananchi anaruhusiwa kuitumia na pale ambapo inahitajika kutwaliwa kwa ajili ya sababu nyingine hasa za maendeleo ya taifa, basi mmiliki wa ardhi hiyo anastahili kulipwa fidia.
7. Nini misingi ya uthamini wa fidia?
· Thamani ya ardhi na mali isiyohamishika (unexhausted improvements)
8.Taratibu za uthamini wa fidia
Uthamini hutekelezwa katika hatua kuu nne:
(a) Maandalizi ya awali (pre-site inspection):
b) Ukaguzi wa mali
· Kuhesabu mazao ili kubaini idadi na kiwango cha ukuaji wa mazao ya aina mbalimbali
) Ukokotoaji wa thamani
d) Utayarishaji wa Hati za Fidia (Compensation Schedules)
Baada ya kumalizika uthamini na kuandaa taarifa,majedwali ya fidia yanatayarishwa yakionesha;
1. Mthamini Mkuu
2. Afisa Ardhi anayeshughulika na zoezi hilo
3. Katibu Kata wa Kata husika
4. Mkuu wa Wilaya husika
5. Mkuu wa Mkoa
Ulipaji wa Fidia
Husimamiwa na Katibu Mtendaji kwa kuwatambulisha walipwaji fidia.
9.TARATIBU ZA UTHAMINI KWA UJUMLA ;
Kwa mwananchi anayehitaji huduma ya uthamini kuna taratibu za utendaji zinazohusisha:-
· Ili kumwezesha Mthamini aifanye kazi yake kwa ufanisi mkubwa, ushirikiano kati ya mteja na Mthamini unahitajika sana. Mteja anapaswa kuwa mwaminifu kwa kujibu maswali mbalimbali atakayoulizwa na Mthamini.
© 2021 All Rights Reserved.
Site Map
Staff Mail
Designed and Developed bylbl_ega_nam (e-GA) and Contents Managed by Ministry of Lands, Housing and Human Settlements Development