Vyombo vya Habari

TAARIFA KWA UMMA

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inaratibu na kuendesha zoezi la kutambua kampuni zote zinazojihusisha na shughuli za Uwakala wa Milki/watu binafsi katika uuzaji/upangishaji wa nyumba/viwanja na mashamba. Hatua hii inalenga kuboresha utoaji wa huduma za sekta ya Milki nchini.